Jumanne, 10 Novemba 2015

MHAZINI WA KANISA NDG:SAMORA KIBOYE AFANYIWA OPERESHENI








Mhazini wa kanisa la shirati central sda ndgu samora kiboye amelazwa katika hospitali ya KMT KABWANA hospitali ya wilaya ya rorya .mhazini huyo wa kanisa mwenye umri wa miaka 35 alianza kuumwa kuanzia  07/11/2015 akiwa dukani kwake mda wa saa 3:00 asubuhi ndipo alipoanza kuhisi maumivu tumboni ilipo fika majira ya saa nne usiku alizidiwa na kufikishwa hospitalini baada ya kupimwa na kugundulika kuwa ana APENDEX   na madktari kuamua kumfanyia operesheni 10/11/2015 mda wa saa 5 asubuhi  ndgu samora kiboye bado yupo chini ya uangalizi wa madktari hadi pale atakaporuhusiwa tuzidi kumuombea

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

WASILIANA NA KANISA

wasiliana na kanisa kwa
E MAIL ADRESS shiraticentralsda@gmail.co
                               BOX 198 SHIRATI RORYA

KANISA YAOMBA AMANI NCHI NZIMA

Kanisa la wasabato la shirati central iliyoko shirati Rorya Mara inapenda kuwapongeza watanzania wote waliyoshiriki uchaguzi wa nchi huku likiomba kwa dhati kabisa Amani kuwepo ndani ya nchi kwani muweza yote ni Mungu ambaye yy ndiye alimuumba kila mwanadamu hata kama aliyeteuliwa kuwa mkuu wa nchi yetu hakuwa chaguo lako lkini tumuombe tu muumbaji wetu Tanzania izidi kuwa na amani na aliyeteuliwa atende kazi huku Mungu akitanguliza fimbo yake mbele yake ili tusiingie ktkt taabu yoyote ktk nchi yetu ndani ya miaka yote mitano ktk uongozi wake wote ndani ya miaka mitano

TUIOMBEE UCHAGUZI WA KANISA

Wapendwa tuendelee kuiombea kanisa kwani tarehe 1/11/2015 siku ya jumapilii  kanisa la shirati central litakuwa na uchaguzi wa watendakazi wa mwaka 2016 Tuzidi kumuomba Mungu achague viongozi wa kanisa wajumbe wa baraza la uchaguzi watumike kama chombo tu. MUngu akubariki saana

Jumapili, 4 Oktoba 2015

TAZAMA UKURASA HUU KUSOMA MUHTASARI MUHIMU WA LESONI KWA AJILI A WIKI HII

SIKU                                                                         SOMO
jumapili                                                                     Historia ya haraka. waamuzi .{2:1-15} ni nni                                                                                              kilichosababisha zahamahii ns ilidhihirishwaje?

Jumatatu------------------------------------------------------Falme mbili:1wafalme12:26-31 je hili linapaswa kutuambia nini namna ambavyo hali ya mambo iliyopo inaweza kupofusha uamuzi wetu kiasi hicho?

Jumanne--------------------------------------------------Maovu mawili:yeremia 2:1-8, soma haya hii yote

Jumatano------------------------------------------------------Tishio la Bbabeli:yere 27:6,yeremia 25:8-12 Ujumbe wa yeremia kwa watu wa yuda ulikuwa upi?

Alhamisi------------------------------------------------Kuapa kwa Uongo;yeremia 5:1,yr 5:2,3 tazama pia law 19:12 Ni mambo gani yanazungumziwa hapa?





ijumaaa JIFUNZE ZAIDI

SOMO LA WIKI HII:ZAHAMA {Ndani na Nje}

soma mafungu haya kwa ajili ya juma hili:Amu 2:1-15,1wafalme 12:26-31 2nyaraka33:9,10:yeremia 2:1-28 5:2,3



FUngu la kukariri Israel walikuwa utakatifu kwa Bwana,malimbuko ya uzao wake:wote watakaomla watakua na Hatia,uovu utawajalia:asema Bwana{Yeremia 2:3

Jumamosi, 3 Oktoba 2015

HIVI NDIVYO SABATO YA KWANZA YA 03\10\2015 ILIVYOANZA

HATIMAYE ROBO YA NNE imeanza rasmi na katika sabato hii ya kwanza iliyoambatana na ibada ya maombi ya kufunga kilianza na mkutano wa waalimu kwa kujifunza mwongozo wa kujifunza biblia(LEASONI> Na baadae muda wa kuimba nyimbo za kikristo ilifuatia kabla ya huduma kuu

Ijumaa, 2 Oktoba 2015

KARIBUNI KATIKA IBADA YA KESHO NDANI YA KANISA LA SHIRATI CENTRAL
IBADA AMABAYO ITAKUWA NI MAALUM KWA AJILI YA KUOMBEA MAMBO MBALIMBALI KWANI KAMA KAWAIDA YA MWANZO AU MWISHO WA ROBO KANISA LETU LINA UTARATIBU WA MAOMBI YA MFUNGO

SOMA MWONGOZO WA KUJIFUNZA BIBLIA KILA SIKU

Bofya hapa ujisomee lesoni yako kila siku katika page yetu hii.
 Ndugu msomaji wa mwongozo wa kujifunza biblia usije ukakosa kusoma lesoni ya robo hii ambayo masomo yote tutakuandalia na kusoma online kupitia website yetu hii
.JIFUNZE ZAIDI UJUE MAANDIKO UBARIKIWE ZAIDI
Ongeza kichwa

Jumamosi, 26 Septemba 2015

KARIBUNI KWENYE KANGAMANO LA KWAYA


Karibuni kwenye kongamano la kwaya litakalofanyika rasmi katika eneo la kanisa la SHIRATI CENTRAL siku ya jumapili tarehe 27/9/2015 kuanzia saa mbili kamili asubuhi.Kwaya lengwa ni Shirati central
Shirati east
Obwere
Bwiri
Mbire
kinyence
kabwana
sidika
sota
minigo
Ryagati
bunyangi na mengineyo
 Kwaya hizi zote zinatoka katika mitaa miwili yaani VICTORIA na SHIRATI njoo ushuhudie mwenyewe waimbaji wakimwimbia Mungu bila hofu na sauti zenye kusikika za kubariki.
Njoo hubarikiwe mpendwa

Ijumaa, 28 Agosti 2015

JINA LINALOOGOPWA NA WENGI.bofya hapa ujue

Katika maisha yako yote jina gani unaliogopa zaidi?
hilo lilikuwa ni swali ngumu katika ibada hii ya leo ndani ya kanisa la shirati central 
soma MATENDO YA MITUME 4:12 uangalie jina lenye faida zaidi kwa watu na linaloogopwa
soma KUTOKA 15:......utazame namna ambavyo Mungu alimshughulikia Farao
mpendwa msomaji tafadhali fatilia mafungu hayo utagundua jina linalohitajika kuogopwa na kuinuliwa watu wote ktk ulimwengu huu

Ijumaa, 14 Agosti 2015

karibuni katika ibada ya sabato ya siku ya leo
    kesho kutakuwa na ibada ya kipekee ya kufunga makambi kinyenche katika mtaa wa shirati.
 kutakuwepo na kwaya mbali mbali ikiwemo kwaya alikwa kutoka obwere katika makambi hayo

Alhamisi, 13 Agosti 2015

HEBU ZITAMBUE SIRI ZILIZOPO KWENYE NAMBA MBALIMBALI KUHUSU MAMBO YA KIROHO

/ZIJUE NAMBA\
Mwanzo 6;14 1korintho2;10 ufunuo 19;10
No 1,maana yake @Mungu ni mmoja, kumbukumbu la torati 6;4
B,kanisa ni moja}efeso 4;4
C,iman ni moja}efeso 4;4
D,ubatizo ni moja efeso 4;4-6,1 korintho 12;13
NO 2,Maana yake kiunabii ktk biblia
@Agano la kale na agano jipya{mathayo 13;31-52
B,watu wawili{mwanamke na mwanaume}kuunganshwa na kuwa mwili mmoja;Mathayo 19;3-6
NO 3 Maana yake:Ushirika wa utatu mtakatfu yaani Mungu baba,mwana na Roho mtakatifu
1 Yohana 5:8
Mwanzo 1:26
2 Korintho 13:14
No4: Maana yake katika biblia
A: Pande nne za dunia
B: Malaika walioshika pande kuu za dunia ili shetani asidhuru dunia mpaka mungu amalze kupiga muhuri wa watu wake Daniel 7:1-2, Ufunuo7:1-3
No7: Ukamilifu wa mungu(siku sita fanya kazi yake)
Ufunuo 6:1,ufunuo 8:1,8:6,ufunuo 1:20,ufunuo10:3
No 12:Ufunuo21:9-24,ufunuo 21:21
No 24:A:Viti vya ukuhani
            B:Viti 24 vinakaliwa na watu 24 ufunuo 4:1-10,Mathayo 27:51
No 30:Ukomavu wa kikohani luka 3:23
No40:Uzoefu wa mambo ya kiroho luka 4:1
Mwanzo 7:17,Mathayo3:1,Yohana 3:1
No 50:Jubeled(mambo ya walawi 25:10
No300:Ushuhuda wa Gidioni Waamuzi 7:19,Ufunuo 17:13

           



                                   KUNENA KWA LUGHA:
TUNAWEZA KUMTAMBUA  MTU AMBAYE ANANENA KWA ROHO?
1:Lazima aweze kufasiri baada ya kunena
2:Lazima mtu asiye wa kabila lake amuelewe
3:Lazima awe amebatizwa kwa roho kama kristo alivyosema.
1Wakorintho  14:6-9 maana kuna lugha nyingi duniani  lakini je kama hakuna roho mtakatifu je twayaweza kuyasikia?
SWALI:Je mtu asiyeweza kufasiri alichokinena anaongozwa na roho?
1Wakorintho  14:10-15 Basi ikiwa tunanena kwa roho tuombe tupewe kufasiri lakini kama huwezi kufasiri basi hujui ulinenalo.
Matendo ya mitume 2:1-12 Siku ya pentekosti wanafunzi walinena kwa roho na hata watu wote wakaelewana.
Mathayo 3:11-12 yeye awabatizaye kwa roho na moto ndiye muweza yote yesu kristo
Je lugha unayoisikia ikinenwa na waganga wachawi na wengine unaisikia?.
Kubali kumpokea kristo ili upate kufunuliwa habari hizi  ZABURI 25:14 Siri yake ameificha kwa wale wamchao tu.


Jumapili, 12 Julai 2015


 BAADHI YA P.F.C KATIKA GWARIDEB LA UFUNGUZI WA KAMBI KATIKA MTAA WA SHIRATI KAMBI LA KATI
NI KATIKA UFUNGUZI WA MAKAMBI MTAA WA SHIRATI KANDA YA KATI